Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, July 29, 2011

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-7



Rose muda wake wa kuondoka ulipofika alijikuta akiwa kachoka sana, na alichofanya ni kuhakikisha kuwa katoa maagizo yote kwa mwenzake anayeingia na hakuishia hapo alikutana na mlizi wa siku hiyo kumpa maagizo yote, na baadaye akakutana na manesi wanaoingia siku hiyo kuwapa taarifa kuhusu huyo mgonjwa maalumu. Na alipohakikisha kuwa kila kitu kipo sawa akarejea pale alipolala yule mgonjwa na kumpima vipimo vyote, na alipofika kumwangalia usoni akajikuta akisisimukwa mwili mzima, …akadharau hiyo hisia kwani hakutaka kabisa hisia kama hizo zimjia akilini, hataki hataki, hawataki kabisa waanaume tena!

Akairudisha hali yake ya kawaida na moyoni akisema, `mmmh, sura kama ya …oh,….shiti…’ akajilaumu kwanini kajikumbusha mbali. Akainama tena wanaume…akainama kutaka kumsikilizia mapigo ya moyo kifuani kwani hakukiamini kipimo chake,…akasimama ghafla na kusema `at last’….hatimaye….wuwuuuu..’ akaangalia vifaaa vya kuangalia mapigo ya moyo na kutabasamu alikuwa anaona mabadiliko makubwa, kuoneysha kuna maendeleo mazuri na huenda mgonjwa huyo akaamuaka wakati wowote…

‘Lakini mabadiliko hayo nimeyaona muda mrefu lakini hakuna dalili yoyote…, cha muhimu ni kuwa anatupa matumaini maana ilifikia hatua tukajua huyu sio wa kuishi tena,…..’ akasema Rose akimkabidhi mwenzake.

‘Anaonekana bonge la `handsome’…hivi atakuwa katokea wapi nan i kitu gani kilimsibu, au ni mmojawapo wa wavuvi wageni waliopotea…au..hapana sidhani kama ni gaidi huyu haonyeshi hiyo dalili’ akasema Dakitari mwenzake akimkagua kagua…
‘Lakini shosti kuwa makini…Mhh, kuwa makini…usijali uhandsome wa hawa watu wote tabia zao ni moja…I hate them, unajua kuwachukuia hawa watu, basi mimi nawachukia ile basi….!..’ Akasema Rose, na mwenzake alimuelewa, ingawaje yeye alishukuru kwani ana mume wake sasa na..wanataraji mtoto..alimuonea sana huruma Rose, hata inapofikia hatu ahiyo ya kuhadithia maisha yake yaliyopita…!

‘Unajua Docta… , majangiri wote wapo hivyo, wakiwa katika mishemishe zao, hakikisha huchezi mbali naye, na humpi nafasi ya kutoka nje…akizindukana tu, simu polisi….’ Rose akamwambia , na kurudi kumwangalia tena usoni, na akajikuta akitabasamu tena, huku moyoni akisema, `whatever… all are the same…’ alijikutwa hana mawazo siku hiyo kwani alikuwa na kibarua kikubwa, kuhudumia wagonjwa na kila mara kuja kumwangalia huyo mgonjwa ana maendeleao gani, …na kila alipojiwa na mwazo alijaribu kutafut aakzi ya kufanya ambayo ilimsahaulisha hayo anayowaza. Hata hivyo alijiuliza sana, kwanini tangu amuone huyoo mgonjwa, akili yake imekuwa kiwaza maisha yake yaliyopita!

Tangu alipofika asubuhi alitaraji atapata muda wa kupumzika kidogo kabla hajaanza majukumu, lakini kilichomshangaza ni kukutana na bosi wake ambaye aliomba sana kwa mungu wake kuwa sikutane naye kwa siku hiyo ya kwanza ya kurejea kazini, lakini hakukuwa na jinsi kwani alitakiwa kujua kazi ipo au la…halafu hata baada ya kuwa na uhakika kuwa kazi ipo akajikuta akibambikwa kazi moja kubwa, ambayo ilihitaji muda wake mwingi kuwa karibu na huyo mgonjwa, kama dakitari na bado kama mlinzi.

`Eti wananipa na kazi ya ulinzi tena, huyu dakitarii kweli hanitakii mema, mimi nitatimiza wajibu wangu kama dakitari na hiyoo ya ulinzi nimewapa maaskari, of-course nitafuatlia kuona hawafanyi makosa ,lakini asitarajie eti nitashinda hapo na hata kulala hapo hospitalini….hiyo haipo kwenye mkataba wetu wa aira, kama hanitaki aseme, nisepe kimbele, nikauze vitumbua…’ akawa anaongea na rafiki yake wakati wanaondoka kwenda nyumbani.

‘Lakini nafikiri umemuelewa vibaya kwani nionavyo hivyo ndivyo ilivyo sizani kwamba kwa vile kakwambia eti uhakikishe unamlinda huyo mgonjwa asitoroke, ina maana ugeuke kuwa mlinzi wake…lakini unamuonaje huyo mgonjwa anafanana kweli na hawo wanaowaita majingiri sijui..au nasikia wana jina lao siku hizi…wanaitwaje vile…ma…magaidi..?’ akauliza mwenzake.

‘Kwani hawo magaidi wanaandikwa usoni, ni watu kama sisi… , lakini wana nyendo zao wana yao wanayopigania. Na watu hawa ni werevu sana wanachofanya ni kuzisoma tabia za mahali na watu wake halafu wanajifanya kama wao ni raia wema kabisa…kiasi kwamba mnakuwa hamna shaka nao tena, na wakiona kuna nafasi ya kufanya hujuma, wanaitumia, unasikia bomu limelipuka mahala usipotarajia kabisa….kwahiyo ndivyo ilivyo…, lakini nilivyomwangalia huyo mgonjwa kwa ujumla na hisia zangu hafanani na watu kama hao, anaonekana mpole, mrembo…yaani wewe hata akiwa kafumba macho unavutia kwelikweli…….’ Akasema Rose huku akiangali hewani kama anajenga hisia fulani.

‘Umeanza,…duh, mungu mkubwa, kukusikia leo ukisema hayo maneno, ama kweli kila jambo lina mwanzo na mwisho wake…naona kabisa akili ya kibinadamu ya kutamani wanaume imekurudia maana tangu yule nduli akutelekeze wewe na wanaume mumekuwa maadui utafikiri jamaa huyo alikaa kikao na wanaume wote duniani kupanga wakufanyie hivyo, …rafiki yangu huwa kila jambo hutokea kwa sababu fulani huwezi jua kwanini ilitokea hivyo, bahati yako haikuwa kwake, wewe angalia ,mbele kama utampata mwingine endelea naye, sasa wewe miaka mingapi unawagomea wanaume wote, hutaki urafiki au uchumba, ina maana umegeuka `mtawa’ shauri lako uzazi utaganda na….’ wakawa wanaongea na rafiki yake na basi walilopanda lilikuwa limeshafika sehemu yao ya kuteremka, lilikuwa basi lao la kazini na wakiteremka hapo huwa wanatembea kidogo kwa miguu kuingia eneo la nyumba yao waliyopangishiwa.

Rose alikuwa katoneshwa kidonda na rafiki yake , hakutaka kabisa kukumbushwa maisha yake yaliyopita, alikuwa keshafikia hatua kuwa yaliyopita yamepita agange yajayo, lakini kila alipokutana na mwanaume akamtamkia kuwa `anampenda’ ile taswira ya maisha yake ya nyuma humjia anakumbuka lile tukio kama vile limewekwa mbele yake na kufunikwa na kitambaa laini ambacho ukija upepo kinafunuka na kuyaona maisha yake yaliyopita….alifumba macho na kumbukumbu za maisha yake ya nyuma zilimrejea tena.

********

Ilikuwa siku ya sherehe ya kumaliza chuo cha Makerere, akiwa kashika shahada yake yakumaliza elimu yake hiyo ya udakitari na ilikuwa nia yake kuendelea zaidi na kufikia hatua ya juu, hasa akiwa kabobea katika maswala ya akili (Neurologist) na nyanja hii aliipenda sana na hata lilipotokea hilo tatizo lililomharaibia mpangilio wake wa kimaisha hakukata tama akawa anajiendeleza hadi akafikia kiwango hicho cha dakitari kamili, lakini lengo lake hasa ni kufikia kiwango cha kuitwa dakitari bingwa `specilist’

Alikumbuka siku ile wakati wakiwa na furaha na kila mmoja akiota ndoto zake kuwa sasa hatua muhimu wameimaliza kilichabakia ni kuingia kwenye jamii na kujichanganya kwa kutoa huduma na matumaini ni kupata marejesho mazuri ambayo yatawafanya maisha yao yawe mazuri. Kinyume na matarajio hayo wengi wao walijikuta wakipambana na mitihani mingi, ukizingatia kipato na kazii hiyo ngumu, na wengi walitupwa kwenye hospitali za serikali zilizopo mbali na mji, na kwenye mazingira magumu…na matokea yake wengine wakakata tamaa kabisa na kazi hiyo na hata kuamua kubadili muelekeo lakini hakuwa kwa Rose, kazi hii ilimkaa kwenye damu.

‘Rose kuna barua yako hii, nimeiona tangu jana, ina maana hukuangalia sehemu ya barua ,maana naiona kama imekua siku nyingi, au hukutarajia barua yoyote karibu!’ Rafiki yake akawa anaingalia ile barua kabla hajamkabidhi rafiki yake na kuendelea kusema ,`…. maana najua baada ya sherehe hii kila mmoja anachukua begi lake anaishia kivyake, huenda imetoka kijijini, hapana hii imetoka Marekani…sio ya inatoka kwa mchumba wako hii…au ndio ajira zinakujia mapema…’ akamwambia rafiki yake waliyekuwa wakichangia chumba.

‘Barua ya nini tena, …unajua meti, hapa akilini mwangu sihisi kitu, akili yangu haipo hapa, hata hiii sherehe ya kumaliza chuo hapa kwangu haipo akilini, mimi ninawaza ndoa yangu tu, maana huyu mchumba wangu alitaka kuwa anashuka uwanja wa ndege anaingia kwenye kufunga ndoa, …na imebakia wiki moja tu, na nilivyosikia kuwa kila kitu karibu kipo sawa, familia yangu wameshapanga kila kitu, nasikia huko nyumbani vigelegele vimeshaanza kusikika…sasa hapa nipo kama sipo’ akasema Rose

Rose akaipokea ile barua na kuiangalia akashangaa mbona mwandiko ni wa mchumba wake, na barua hiyo inaonekana ilifika wiki mbili zilizopita, kwa tarehe ile inaonyesha ilifika kipindi wakiwa katika mitihani migumu, …labda walimu waliamua kutotoa barua yoyote wakati kama ule, wakiwa katika mitihani hiyo, ili isije ikawaharibia mazingatio yao…labda…lakini tangu afike hapo itakuwa mara ya kwanza…na akashukuru kuwa ni barua toka kwa mchumba wake,…ambayo hatarajii kuharibiwa mazingatio yake… labda ilikuwa na maneno ya kumtakia maandalizi mema ya mtihani na ndoa inayokuja…akaishika na hakuwa na haraka nayo kuifungua, akasema moyoni barua kama hii inatakiwa unaisoma wakati upo kitandani umejipumzisha, haihitaji haraka, …kwani maneno mengi yatakuwa ya kimapenzi…na anamjua mpenzi wake anavyojua kuandika hayo maneno, unasoma huku unasisimukwa na mwili mzima…utafikiri mpo naye karibu …mnaonngea naye mmmh, akaguna huku akiiangalia ile barua….

‘Nitaisoma baadaye ,… wakati huu ni wa kupumzisha kichwa, kidogo, mtu uoge ujiande na huko mnakokuita kujirusha, mimi sina hata hamu ya kwenda huko ukumbini, lakini kwa vile ni siku ya moja muhimu ya kumbukumbu itabidi niende tu…maana nitawahadithia nini wazazi wangu ikizingatiwa kuwa wapo mbali na hakuna hata jamaa yangu aliyebahatisha kuja hapa kushuhudia sherehe hii, kwahiyo nahitaji kila hatua niiweke kwenye kumbukumbu zangu…na ni vyema nipate kumbukumbu sahihi kwa ajili ya kwahadithia wazazi wangu na hasa mchumba wangu…’ akasema Rose

‘Mhhh, mchumba wangu, mchumba wangu, unanikifu na hiyo kauli, utazania wewe tu ndio …lakini nakuonea wivu sana, maana siku hizi kupata mchumba nako kazi kweli…. , halafu ndio umpate na mfikie hatua ya ndoa ni jambo la kushukuru sana, wengi huishia kuzalilishwa na kupata watoto bila kuwepo kwenye ndoa, …hilo kwangu nalipinga sana, nataka mtoto anafaidi ndoa ya wazazi wake, anazaliwa anakuta wazazi wake wapo kwenye ndoa, na sio anakuja kukutana nayo….sijui unanielewa maana ukisema hivi watu wengine wanakuelewa vibaya, …lakini mimi ndio msimamo wangu….’akasema rafiki yake.

‘Sio msimamo wako, ni msimamo wa kila msichana, kila mwanamke, kuwa anaolewa, halafu wanapata watoto, sio wanapata watoto ndio wanaoana…lakini wengine inatokea kinyume chake, kwasababu sijui ni wanaume wadanganyifu au ni kujisahau au ndio huko kupimana kizazi…hata sielewei, lakini yote ni mtu na kili yake…hilo nakuunga mkono, hata mimi nilishamwambia mchumba wangu yote yatafanyika baada ya ndoa, na hili lilikuwa likimuumiza sana,…akija likizo anakuja akiwa na mambo ya kizungu-zungu, siunajua tena wenzetu hawo waliosomea nje, wanataka kila kitu kizungukizungu…mimi nilimwambia `no way’ hapa kwangu ni `ubantu’ kwa kwenda mbele, …’ akasema Rose huku wanaingia kwenye mabweni yao ya kulala...

‘Naona tuapte nusu saa ya kulala kidogo, halafu tuoge, baada ya hapo…nina wazo usivae kwanza, wewe lete nguo zako chumbani kwangu, tusivae kwanza tuchague nguo gani inafaa kwa siku ya leo,…nitakusubiri kwangu…’ wakakubaliana na wao walipata bahati sehemu wanayokaa ina vyumba viwili na varanda katikati, na bahati njema hakukuwa na wanafunzi wengi kwahiyo kila mmoja alilala kwenye chumba chake na kuchangia varanda…

Ilishapita saa moja na rafiki wa Rose hakuona dalili ya kutoka nje kwa rafiki yake, na hakumbuki kumsikia akioga, yeye alipopata usingizi kidogo na baadaye aliamuka na kuimwagia maji ,alipomaliza kuoga, aliingia chumbani kwake akawa anatafuta nguo za kumuonyesha mwenzake, na alipomaliza kwa vile waliahidiana kuwa Rose ndiye atakuja kwake, akawa anamsubiri…huku akitizama kitabu chake cha picha, akasubiri wee kimiya, akapanga vitu vyake na kuona ngoja yeye achukua baadhi ya nguo zake amwendee mwenzake chumbani kwake….

‘Rose vipi wewe , ndio maandalizi gani hayo, nimekumbia uje huku kwangu kwanza tukaguane wewe kimiya…aaah, tabia hiyo mimi siitaki…haya mimi nakuja huko kwako…’akawa anasema kwa sauti, lakini hakusikia mwenzake akijibu. Akashikwa na mshangao akaita kwa sauti `Rose, Rose…..’ kimiya, akafunga mlango wa chumba chake na kuelekea chumba cha rafiki yakke huku akiwa kaingiwa na wasiwasi, sio kawaida ya rafiki yake kuwa hivyo, wakiahidiana jambo yeye huwa wa kwanza kuhakikisha kuwa kalitekeleza, sasa imekuwaje, au ndio kapitiwa na usingizi…haiwezekani!.
Akafungua mlango wa rafiki yake bila hodi akiwa na hasira na wasiwasi…`wewe mwanamke mbona….’ Alishikwa na mshangao, na nguo alizokuwa kazishika mkononi zote zikamdondoka chini na kushika mdomo kuzua sauti,…lakini haikuwezekana, alijikuta akipaza sauti kwa guvu akisema akisema `heeelp..jamani help…..’

NB: Imekuwaje jaje…mmmh, nashindwa kuenedleza zaidi maana leo ni Ijumaa, natakiwa kumalizia kazi za siku, na sehemu hii nimeiandika harakaharaka leo , ili angalau kusiishe siku bila kuandika chochote, nahisi kuna makosa mengi mnisamehe kidogo….TUPO PAMOJA

20 comments :

Anonymous said...

wewe nimekuvulia kofia, huna mfano mkuu

Anonymous said...

Ntakutumia email address yangu kwenye email yako. wala haina makosa imekaa vizuri.

Subira

samira said...

we acha jamani mhh nangoja next week have a nice week end m3

DIGITAL WORLD PAGES ARCHIVE said...

Hello! Nice to meet You! Very interesting...

Pam said...

ucombe kutendwa pole Dr Rose.

Anonymous said...

Have yοu ever thought about adding а little bіt moгe
than just your аrtiсleѕ? I meаn, what you say іs valuablе and еverything.
Hoωever just imagine if уou added somе great pіcturеѕ or
video clips to give уour posts mοre, "pop"! Your content is excellent but
with іmаges anԁ clips, this sitе сould certаinly be one of the greateѕt in its field.
Wonderful blog!
My page : Colon Cancer

Anonymous said...

What's up everyone, it's my first pay a quick visit at this site,
and paragraph is really fruitful designed for me, keep up posting these types of articles.


my web page :: cialis

Anonymous said...

Thе report hаs eѕtablished benefiсial to me personally.
It’s extremely useful and you really are
obviously really wеll-informed of thіs tyρe.
Үou have еxposеd my personal eye in orԁeг to differеnt thoughts abοut this particular
matter with interestіng and reliable wrіtten content.



Checκ out my blog post :: buy viagra
Feel free to surf my web blog ; viagra

Anonymous said...

Τhе repοгt offers
proven helρful to me pегsonally.
It’ѕ rеallу uѕeful аnd you're simply certainly quite educated in this region. You have popped my own eyes for you to numerous opinion of this kind of subject along with intriguing and sound content.

Also visit my web page Buy phentermine
Also visit my web blog ; buy phentermine

Anonymous said...

Hi there, thе whole thіng іѕ going sounԁ here and
ofcourse everу one iѕ shагing factѕ, that's truly good, keep up writing.

my blog - payday loans

Anonymous said...

Hello Therе. I founԁ your blog using msn.
This is an еxtremеly wеll wrіtten article.
I'll be sure to bookmark it and return to read more of your useful information. Thanks for the post. I'll definitеly comеback.


Нere is my wеblog - payday loans

Anonymous said...

Your own post haѕ confіrmed bеneficial tо uѕ.

It’ѕ quite useful and you aгe сertainlу verу educаtеd in this field.
You have got opened up my pеrsоnal faсе tо bе аble to
variоus opіnion of this specific subϳeсt together wіth intгiquing, notable and ѕоlid content material.


Chеck out mу blog post; Viagra

Anonymous said...

Yοuг write-up prоviԁeѕ proven necessаry tο myself.
It’s quite useful аnd yοu
really are clearlу rеallу expeгienced in this
region. You possеss opened my sight to be able to numerouѕ thoughts аbоut
this рarticular subjeсt using intеresting and solid cοntent mateгial.



Feel free to visit my homepage ... soma

Anonymous said...

What's up to all, how is all, I think every one is getting more from this web site, and your
views are fastidious in support of new viewers.


Also visit my web blog ... ambien

Anonymous said...

This piece of writing is actually a good one it helps new the weeb people,
who arre wishing in favor of blogging.

my website; You Can Try This Out

Anonymous said...

Great blog here! Also your web site loads up fast!
What host are you using? Can I get your affiliate link to your host?
I wish my web site loaded up as fast as yours lol

Here is my site :: Gestao de documentos

Anonymous said...

Добро пожаловать в блог юмора!
Ежедневные обновления http://koro4.com

Картинки с надписью,искрометный юмор и никакой политики!
Загадочные истории,интересные факты,короче все самое лучшее только у нас на koro4.com
Анекдоты,байки,афоризмы,лучшее авторские работы koro4 лучшее всех.
Различные розыгрыши,юмористические комменатрии короче не бывает.
Максимально коротко но с максимальной полезной информацией koro4.com не бывает.
Добавляйте свои новости,отчерки,записки поднимите настроение себе и другим.
Рисуйте свои Картинки с надписью от koro4.com
Анекдоты,факты,юмора,приколы,прикольные Картинки,офигенный юмора.
http://koro4.com

Anonymous said...

I know this website gives quality based posts and other stuff, is there
any other web site which provides such stuff in quality?

Anonymous said...

I really like what you guys are usually up too.
Such clever work and coverage! Keep up the excellent works guys I've incorporated you guys to my own blogroll.

Anonymous said...

First of all I want to say great blog! I had a
quick question which I'd like to ask if you do not mind.
I was interested to know how you center yourself and clear your
thoughts before writing. I have had trouble clearing my mind in getting
my ideas out there. I truly do take pleasure in writing but it just seems
like the first 10 to 15 minutes are usually wasted simply
just trying to figure out how to begin. Any
suggestions or tips? Thank you!