Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, March 10, 2010

Umri unakwisha na mengi

  Ilikuwa saa saba na nusu, nikiwa ndani ya ofisi moja , mbele yangu alikuwa kakaa bosi wa hiyo kampuni. Mara mfanyakazi wa huduma akaingia akiwa amebeba vyakula toka hoteli za kisasa. Nasema za kisasa manake vyakula vilikuwa vimefungwa vizuri. Hapo mate yakaanza kunitoka, siunajua tena ukiwa umefunga mkanda wa hali ngumu. Bosi Yule akaanza kula na kushushia na vinyaji huku akiperuzi laptop yake. Hakuna cha karibu hapo, tumbo linanguruma kwa njaa!


‘Vipi huendi lunch?’ bosi akaniuliza

‘Mhh, nilitoka kidogo, mmh…’ nikajiumauma nikiogopa kusema ukweli kuwa nimefulia, tangu asubuhi sijapata chochote zaiidi ya chai ya asubuhi.

Nikakumbuka swali liloulizwa kwanini umri wa Mtanzania kwa wastani unakuwa chini ukilinganisha na wenzetu wa mataifa yenye nacho! Majibu yapo mengi, sio ya kubahatisha.

Angalia hali za ofisini, wenye makampuni wanajua wanachokupa hakitoshi, wao wanachokulipa ndio matumizi yake ya siku mbili. Hali hii inawafanya wafanyakazi wafanye kazi kwa shida, njaa na kukata tamaa, na wengine huzidiwa na hatimaye kufanya kinyume na taaluma zao. Na mwisho wa siku umri unapungua.

Ilipofika jioni, nilishukuru mungu na kuharakisha kukimbilia kituoni. Nilipofika nilikata tamaa, kwani umati uliokuwepo utafikiri Dar nzima imehamia hapo. Nilijipapasa mfukoni kuangalia kuwa nauli ipo, angalau nitembee hadi vituo vya mbele ili nipata gari la kugeuza nalo. Hapo ina maana nilipa nauli mara mbili, nikaona nauli haitoshi. Nakakaa chini ili nisubiri bahati ya kugombea. Nilikaa karibu masaa mawili nikisubiri gari na bahati hilo likaja limeshajaa, lakini bado konda anaita watu kwa kusema kuna siti za kumwaga, ikawa kukuru kakara hadi nikapenya ndani. Oh, nilivyosimama hakuna cha kugeuka au kusogeza mguu, haya twende.

Fikiria hali kama hii, tumejazwa kama magunia, ukipumua unapumua kama sio mgongoni kwa mwenzako ni usoni kwake, na ukikohoa,…ohoo, inabidi uzibe mdomo. Waliokaa walikuwa wakilalamika kwani sie tuliosimama tulikuwa tukiwasonga hata kuwaangukia, utafanyaje nawe upo bongo. Kwa hali kama hii lazima umri utakuwa unapungua. Utapungua kiafya, kwa kuambukizwa magonjwa au hali ya hewa inavyokuwa nzito.

Wakati nawaza haya tukasikia mtoto akilia, alilia kiasi kwamba kila aliyekuwepo alimuonea huruma, ilibidi waliokaa dirishani wampishe Yule mama, ili Yule mtoto apate hewa. Na si huyo tu kukawa na mama mmoja mwenye presha alizidiwa hadi akaanguka ikabidi walikaa wampishe akae karibu na dirisha, safari ikawa inaendelea.

Nilikumbuka asubuhi nilivypata shida ya usafiri, nikiwa na watoto ambao niliongozana nao ili wawahi shuleni. Nilikataliwa kila gari lililopita eti kwasababu nina wanafunzi. Ilibidi niwalipie nauli ya wakubwa ndio tukapata kuondoka. Haya ni matatizo tunayopambana nayo asubuhi kabla hujafika kazini, achilia mbali ada, nauli na mengineyo, haya yanachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza umri wetu! Hapa jikumbushe na tukio hili la adha ya usafiri dar

Labda tujiulize kama ndio hivyo tufanyeje. Nakumbuka niliwahi kufanya kazi kwenye kampuni iliyokuwa ikitoa chakula kwa wafanyakazi., na ilikuwa na mpango wa kununua gari la wafanyakazi, kwanini hii isifanyike kwa kila kampuni? Utakuta meneja ananunuliwa gari la hela nyingi tu, mshahara wake mkubwa watoto wake wanasomeshwa, sasa wao ni nani na wewe ni nani. Kwa kufupi wao ndio wao na wewe ndio wewe. Umri unakwisha ukizidi kuwaza hayo!

From miram3

1 comment :

Anonymous said...

Wewe unanichekesha kweli sasa ulitaka bosi ukukaribishe wakati kaagiza chakula kiasi chake? Nyie ndio mnaoenda kwa watu na kudai mwenye nyumba awakaribishe chakula wakati hukuwekwa kwenye bajeti