Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, February 12, 2010

Tatizo ni kufaulu mitihani?

‘’Wewe umepata divisheni ngapi” Lilikuwa swali la wengi wakiulizana ndani ya `internet café’ moja niliyoingia kuandika mambo yetu. Wale waliofanya vizuri walijibu kwa sauti, ni haki yao kuonyesha ulimwengu kuwa wamefaulu mitihani. Lakini wapo wale waliofeli au kupata chini ya kiwango, hawa walikaa kimya kujibu au wengine walidanganya kuwa majina yao hayaonekani!


Wakati nawasikiliza hawa vijana waliojaa mle ndani kwa shauku, nilijaribu kujiuliza lengo hasa la mitihani hii ni nini, na je linakidhi haja ya watoto wetu? Nilicheka pale nilipotamani kumuuliza mzazi mmoja aliyekuwa akimgombeza mtoto wake kuwa amemuabisha kwa kupata chini ya kiwango.

‘Nimepoteza hela zangu nyingi kwa tuisheni, na kila kitu nilikupa sasa ndio nini hiki umefanya’ alilalamika Yule mzazi. Pembeni yake alikuwepo mama mmoja aliyejaa furaha kuona mtoto wake amefaulu vizuri, na hakusita kumshauri mwenzake kuwa kufeli sio kwamba mtoto wake alikuwa hana akili, lakini mitihani wakati mwingine inaweza ikaja kinyume na mtoto alivyojiandaa! Nikashangaa kidogo kusikia kuwa `kuna jinsi mtoto anavyotakiwa kujiandaa’

Hebu tujiulize kama wazazi mfano mtoto wako kipindi chote cha miaka mine aliyokaa shule hakuwa akifanya vizuri katika masomo na ghafla katika matokleo yake haya ya mwisho akawa amefaulu vizuri , wewe kama mzazi utasemaje? Na pia tuchukulie wewe mtoto wako alikuwa akifanya vizuri katika masomo yake, na kila mara anakuwa wa kwanza darasani, lakini mtihani huu wa mwisho akawa amefanya vibaya, wewe kama mzazi utasemaje, nahisi unaweza hata ukalaumu kuwa kuna jambo limefanyika kumfanya mtoto wako asifaulu na hata kukata rufaa!

Mimi nahisi kuwa ni bora tukawa tumewaandaa watoto wetu vyema, ili hata kabla ya mtihani watoto wetu wawe wameshafulu. Watoto kama hawa sidhani mtihani wao wa mwisho utakuwa ni tatizo, hata kunagalia matokeo itakuwa ni wajibu tu. Hawa ndio watakuwa wataalamu wetu, kwani maandalizi yalishafanyika mapema, nini alichofundishwa kilishafanyiwa kazi, na mtihani wa mwisho inakuwa kama marejeo ya kupima kile alichojifunza.

Wapo watoto waliokuwa wakienda shule kwasababu wanalazimishwa na hawakujua nini umuhimu wa elimu kwao, wengine walikwenda kwasababu baba zao wana uwezo na wakawa wakionyesha nini wazazi wao walicho nacho, bila kujali juhudi za wazazi wao. Hawa walifikia hata kuwadanganya wenzao ili wajiunge nao katika pilikapilika za starehe, na masomo kwao ilikuwa kama kupoteza muda. N hawa wanahamu ya kuangalia matokeao yao , na furaha yao ni kufaulu. Sasa fikiria mtoto kama huyu akiwa amefaulu, nini taifa letu litaraji baadaye!

Elimu ni muhimu sana, na kama ingefaa ilihitajika kila mtoto asome hadi chuo kikuu, ili aweze kuonyesha nini anachokijua. Nina imani kila mmoja ana uwezo Fulani, kama sio wa fani hii itakuw ya fani fulani ambayo ianweza ikaleta tija kwa taifa na kwa maisha yake mwenyewe, sasa ni bora elimu zikalenga taaluma. Ni bora vijana wakapimwa bado wakiwa wadogo nini wanakijua zaidi ili waweze kukisoma na kukifanyia kazi na tusiwaburuze watoto katika kukariri tu.

Nikiwa bado natafakari nikasikia mzazi mmoja akijisifia kuwa mtoto wake amefaulu vizuri , na anajua kuongea kiingereza kama mzungu. Nilimuuliza hesabu na Sayansi amepata ngapi, akasema katika masomo haya hakufaulu kwa kiwango kikubwa lakini kwa ujumla amefaulu.`Ukiongea naye utafikiri unaongea na mzungu’ akamalizia Yule mama. Mimi nilimpa hongera sana
From miram3

No comments :