Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, September 30, 2009

YOTE MAISHA

Katika kitabu nilichokuwa nakitunga nyuma kidogo kilianza hivi:
                                                            
  Ingawaje nilijitahidi kujizuia kama wasemavyo watu ‘jikaze kiume’, lakini akili na mawazo yangu yote hayakuweza kuhimili yale yaliyonisibu. Mawazo yangu yote yalikuwa yakitafakari tukio zima na jinsi lilivyotokea, yote ilikuwa kama ndoto. Licha ya kuwa kimwili nilionekana nipo, lakini akili na mwili havikuwepo. Nilijikuta nikishikwa begani na mikono iliyokakamaa na yenye nguvu huku sauti kali ya kiasikari ikiniamurisha nisimame.


 `Nisimame niende wapi’ nilijiuliza akilini.

 Nilijizoazoa huku nikichelea kudondoka kwa kosa nguvu za miguu, na bila kutegemea niligeuza kichwa upande ule wa wawatazamaji na macho yangu yalitua pale ilipokaa familia yangu. Nilijaribu kukodoa macho ili niwaone vizuri, kwani kiwingu kizito kilishaanza kutanda machoni. Wote walijaa simazi na kilichonigusa zaidi ni mtoto wangu mdogo ambaye alionekana akiniangalia bila kupepesa macho, sijui alikuwa akifikiria nini.

 ‘Twende hukuu wewe…’ Sauti iliamurisha na sikujua ‘huku’ ilikuwa na maana gani, kwani kilichoamuliwa pale mahakama  hakikutua akilini, sikuwepo kifikira, lakini lakini hisia na nini kilichonileta hapo zilinituma kuwa kwa  vile leo ilikuwa siku ya kusikiliza kama ninaweza kupewa dhamana au la, basi huenda dhamana imekataliwa. Ndivyo hali ilivyoonyesha na ndio habari zenyewe. Nilijua sio rahisi kupewa dhamana ingawaje ilikuwa ni haki yangu.

  Nilijaribu kugeuza macho yangu tena ili niwaone wanafamilia lakini kilichokuwa mbele yangu ilikuwa uwingu wa wandishi wa habari wakichukua picha zangu, na wengine wakijaribu kuniuliza hili na lile, lakini sikuweza kuwajibu, nisingeweza kuwajibu kwani tukio zima lilitokea haraka na ili niweze kujieleza vyema ilihitaji muda wa kutafakari. Ilihitajika nguvu ya ziada kujitetea na nguvu ya ziada zaidi kuishawishi jamii inielewe kuwa yaliyotokea sivyo ilivyo.

  Wakati natembea kutoka kwenye chumba cha mahakama, huku nikisindikizwa na askari wawili mawazo nayo yalianza kutafakari yote yaliyonikuta, huku nikiwa siamini kuwa hayo yote yalinisibu mimi.

NB Ni kisa cha kupambana na maisha,hasa unapotaka maisha yako yabadilike haraka kutoka hali duni kwenda matawi ya juu. Ili ufike kileleni kuna vikwazo, kuna njama, kuna uhalifu nk, na wengine huamua kutumia udhaifi wa wengine kudandia juu, na hawa ni wengi wa matajiri tulio nao . Vyovyote iwavyo, tajiri na utajiri wake,masikini na watoto wake, na yote tunayafanya, ya heri na dhuluma, hutendeka ndani ya maisha yetu,ndio maana tunasema, YOTE MAISHA.
 From miram3

No comments :