Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, August 21, 2009

VITENDO NI BORA KULIKO MANENO

Katika utendaji wa kazi kuna sehemu mbili, kufanya kazi na kazi ijieleze yenyewe, au kufanyakazi na wewe uielezee ile kazi, ama kwa mkubwa wako au kwa jamii. Hii sehemu ya pili wengi ndipo walipo, mtu hawezi kufanya kitu bila kujisifia, bila kujitangaza, bila kujionyesha kuwa ndiye aliyefanya au anajua, na wengi wa watu hawa wapo kwenye siasa.
Mimi sio mwanasiasa,ila ninaikumbuka hadithi ya babu yangu kuhusu milki moja ya majigambo. Mkuu wa nchi ile alikuwa na washauri wake wawili, hawa walikuwa wakipewa kazi mara kwa mara za kufuatilia mambo ya utendaji na mwisho wa siku huleta taarifa.
Watendaji wake wawili hawa walikuwa wajuzi kila mmoja kwa nafasi yake. Mpole alikuwa akifuatilia na kufanya kazi yake kimya kimya, na mwisho wa siku hupeleka taarifa na kumkabidhi bosi wake,ama kwa kupitia katibu muhtasi wa bosi au wakati mwingine kupitia kwa mwenzake ambaye alikuwa Chakaram kwani Chakaramu anajua kuielezea kazi kama alikuwepo.
Chakaramu alikuwa mjanja, yeye huitumia nafasi ya wengine kufanya kazi yake na kwa uchakaramu wake aliweza kupeleka taarifa nyingi kwa bosi wake kuliko Mpole,kwahiyo bosi wake alikuwa akimtumia sana katika kupata taarifa. Watu kama hawa ndio wamejaa maofisni kibao, maneno mengi, lugha utafikiri kazaliwa huko,lakini…ok ngoja tuendelee.
Likatokea lakutokea,kuna mtu kauliwa, na taarifa zikafika kwa bosi, Chakaram na Mpole wakambiwa wafuatilie, Mpole kama kawaida yake akaifanya ile kazi kwa umakini zaidi akijua ule ni uhai wa mtu na kugundua ukweli,na ukweli huo ulimuumiza sana na akaona ni heri aufiche kwanza ili kwanza awe na uhakika nao. Kwa minajili hiyo akajenga hoja ya kuwa huenda aliyekufa alijiua mwenyewe. Na hii akainasa Chakaramu, akaitenhenezea hoja yenye ushahidi kabambe mwisho wa siku akaipeleka kwa bosi wake.
Bosi wake akaisikiliza,na ushahidi alioletewa, kiasi kwamba aliridhika, na kumsifia sana jamaa, kimoyoni akasema duu jamaa huyu ni mkali, huyu ndiye ananifaauyu ninayemuamini kaniletea ushahidi huu basi sina wasiwasi,jamaa atakuwa kajiua.
Bosi akataka kujua kutoka kwa mshauri wake Mpole. Mople alipofika,kama kawaida yake,akafika kwa katibu muhutasi na kumwambia kuwakesi hiyo ina utata, na anahitaji muda wa kuifanyia kazi. Kitendo hiki kilimuudhi bosi,kwasababu muda ulishatolewa na kwanini mwenzake aweze kuleta matokea yeye ashindwe. Jamaa akafukuzwa kazi.
Licha ya kufukuzwa kazi alifilisiwa na akawa katika maisha magumu. Hatimaye siku ya mwisho aliyoomba apewe kutoa taarifa yake ilifika. Aliomba siku hiyo wawepo wazee wa baraza, na hakimu wa-nchi.
`Ndugu Mheshimiwa, nilisita sana kutoa taarifa yangu kwasababu mdomo kutamka ni rahisi,lakini kile unachokitamka sio rahisi kujielezea,lakini kama utaacha kile ulichokitamka kijielezee ni bora zaidi, hakuna haja hata ya kuinua mdomo. Bosi najua unajua muuaji ni nani, labda tumiite shahidi yangu wa kwanza ambaye ni Mheshimiwa mkeo. …’’ Watu pale wakashangaa,iweje. Na mke wa raisi inasadikiwa kapotea kimijiuza.
Ni kesi ndefu kidogo, nitaielezea kwa undani baadaye. Lakini alichotaka kunieleza babu yangu ni kuwa wakati wote, hakikisha kazi na majukumu yako uliyopewa unayatenda kwa vitendo na ukiyatenda ipasavyo yatajieleza yenyewe, usipende mara kwa mara kutumia mdomo kuielezea kazi yako,iache kazi ijielezee yenyewe, akiwa na maana kuwa vitendo huwakilisha ukweli kuliko maneno. Huu ni ujumbe wangu wa leo tarehe 21-08-2009 Je w ewe mwenzangu wasemaje?
From miram3.com

No comments :