Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, August 18, 2009

MWANGALIE ALIYECHINI YAKO

Mwisho wa wiki hii nilienda hospitali, mke wangu alikuwa anaumwa na hali tuliyomchukua nayo nyumbani ilikuwa sio nzuri, kiasi kwamba tuliona tukifika tu tusikae foleni,tuingie moja kwa moja kumuona dakitari.
Wakati tunasubiri kuingia kwa dakitari,kwani tulikuta ana mgonjwa , ghafula wakawa wanaletwa wagonjwa aina kwa aina, na hali zao zilikuwa taabani, ilibidi tuwapishe wamuone dakitari kwanza, licha ya hali ya mke wangu ilivyokuwa, lakini kwa kipindi kile alionekana hajambo ukilinganisha na hao wagonjwa walioletwa.
`Vipi unajisikiaje mke wangu’ Nilimuuliza akiwa ameniegemea
`Najisikia sijambo’ alisema, lakini sauti yake ilionyesha udhaifu kuwa sio kweli hajambo ila alivyowaona wenzake walivyo alijiona yeye hajambo.
Ni ukweli usiopingika kuwa ukitaka kujipima na matatizo yako ni vyema ukaangalia yule aliye chini yako, na ukitaka kujipima kiuchumi kimaendelea ni vyema ukaangalia aliye juu yako. Lakini wengi wetu tunapenda kuangalia juu,kiasi kwamba vichwa vimeganda kuelekea juu, na hii ni hatari.
Dunia ya sasa hivi ni ya papa mkubwa kuwameza samaki wadogo, hakuna cha huruma wala mapenzi. Wale wenye uwezo wanatamani wapate zaidi na hata kama hawakihitaji, kwasababu alieye nacho anazidi kuongezewa na hali yule asiye nacho anazidi kunyang’anywa hata kile kidogo alicho nacho. Jifikirie wewe uliyejaliwa ni mara ngapi umemwaga chakula jalalani, ni mara ngapi umechoma nguo kwasababu haziendani na wakati !
Ushauri wangu wa leo tarehe 18-08-2009 ni kuwa tujitahidi sana kuwaangalia wale walio chini yetu, ili tuwakwamue waje sawa au karibu sawa na sisi kwa kufanya hivyo, hatutasikia vilio vya njaa, hatutasikia vilio vya mwiziii, na kitakachotawala ni upendo, na amani kwani hata yule aliyezidiwa itafika muda atasema `aah, mimi sasa sijambo’

From miram3.com

No comments :